Habari yako na
kukaribisha sana ndugu yangu mpenzi katika blog hii, kama lilivyo lengo kuu la
kuanzishwa kwa blog hii ni kukuonyesha wewe na kukufunza ni namna gani ama ni
njia zipi ambazo unaweza kuzipita ili kuweza kufanikisha malengo yako katika
maisha haya. leo hii kwa ufupi kabisa nataka nikupe nukuu muhimu sana kutoka
kwa mtu mmmoja maarufu sana aliepata mafanikio makubwa sana katika maisha yake.
Na nukuu yenyewe ni hii
hapa “ A dream doesn’t become reality through magic. It takes sweaty,
determination and hard work”. Haya ni maneno ya msingi kabisa na ni machache
aliyoyasema Bwana Colin Powell. Inapaswa kuyaweka kwenye akili yako.
Maneno, haya yenye
maana ya kwamba ndoto haiwezi kuwa ya kweli kama ni uchawi tu au kwa lugha
nyengine tuseme kama ni miujiza tu imetokea au ni bahati mbaya tu kutokea ni mfano kama umeamka asubuhi
ukakuta mvua inanyesha. La hilo haliwezekani ata kidogo.
Lakini tukiendelea
mbele na maneno haya yake yaliojawa na hekima na busara zisizo na kifani
anasema kwamba ni lazima uchukue hatua ambazo zitakuwezesha uweze kufikia ama
kuitimiza hio ndoto yako kwa mafanikio makubwa kabisa.
Kwanza kabisa lazima
ikutoe jasho hapa ana maana gani, kilicho kusudiwa hapa ni kuwa ufanye juhudi
za kivitendo kabisa ambazo ni hatua muhimu za kivitendo utakazo zifanya ili
uweze kuyafikia malengo yako ambayo ndio hizo ndota zako maishani mwako.
Pili, lazima ufanye
maamuzi tena yenye hekima na busara kabisa ni muhimu kuzingatia kwamba kama
wewe unataka ufikie hatua ya kweli kutimiza ndoto zako ni lazima ifike wakati
na uaamue kuwa sasa nitawacha kila nilicho nacho ambacho hakina kwangu mimi
faida yoyote ila kunipotezea muda tu.Hii ni hatua muhimu
kabisa kusema yaliopita tayari yameshapita na sasa nataka kufungua ukurasa mpya
kabisa wa maisha yako ya sasa nay a baadae maamuzi yako utakayo yafanya hapa
ndio itakua hatua muhimu kabisa kutekeleza ile hatua ya mwanzo tuliopita.
Muhimu na cha
kuzingatia katika hatua hii ni kuanisha yale matarajio yako katika maisha yako
na malengo yako kwa uwazi kabisa ni kitu gani unakusudia kukifikia ama una
kilenga katika kufika ukomo wa maisha yako.
Ni lazima uamue hapa
unataka kuwa nani na unataka kuwa na muelekeo gani katika maisha yako lakini
pia hapa uamue unataka kumilika vitu gani kwa mujibu wa hayo malengo yako na
matarajio yako uliyo ya kusudia maishani mwako.Katika kufanya maamuzi
yako inakubidi ni lazima upime na kuichambua ndoto yako na uhalisia wako wa
maisha yako, mazingira yako pamoja na fursa nyingi zilizo nazo unazo zijua na
zile ambazo una lenga kuzijua ili kuweza kuyafikia malengo yako.
Fanya utafiti wa
kutosha kwa kile unachotaka kukiamua lazima uwe na maarifa ya kutosha kwa hicho
unacho taka kukifanyia maamuzi ili uweze kukijua vya kutosha. Kama ni biashara
lazima ufanye utafiti wa kupata taarifa za kutosha kuhusiana na hio bidhaa yako
pamoja na soko lake kwa wakati huo kwa ujumla.
Tafuta ushauri wa kutosha
kwa watu mbali mbali khususan wale waliofanikiwa mnaofanana kwa hicho
unachotaka kukifikia wewe. Unaweza kusoma vitabu vyao ama makala mbali mbali
zinazohusiana na maisha yao au uchambuzi mzuri wa nadharia zao walizozitoa
katika maisha yao.
Vizuri sana ukaamua leo
ni vipi uantaka kuwa ili uweze kuianza safari yako mpya ya maisha yako yenye
kulenga kufikia na kuzimiza ndoto zako kumbuka hakuna atakae kuja kukuamulia
wala kukupangia jinsi gani ya kuamua bali ni wewe mwenyewe utekeleze hili
jukumu lako la msingi.
Mwisho anasema ni
lazima ufanye kazi ngumu akimaanisha ufanye kazi ya kweli kabisa na hapa
unapaswa kujitolea kivilivyo kabisa wala sio kwa kubahatisha au kufanya mchezo
na masihara katika hatua hii.
Lazima ufanye kazi ya
kweli kabisa katika kufikia malengo yako na inakupasa kabisa kuutumia muda wako
vizuri sana kwa nidhamu ya hali ya juu kwa kuhakikisha kila muda unaokufikia
lazima ujue ni hatua gani unaipita ili kurahisisha kuyafikia malengo yako.
Fanya kazi kwa ari na
bidii kubwa ili uweze kufanikisha malengo yako leo, chukua hatua hizi sasa ili
uweze kufanikisha malengo yako leo amini kwa jitahada zako na maamuzi yako ndio
nyenzo muhimu za kurahisisha safari yako ya kutimiza ndoto zako.
Tafadhali endelea
kutembelea na kusoma makala nyenginezo muhimu kabisa zitakazo kuwezesha
kutimiza kwa ufanisi ndoto zako maishani mwako. Zingatia haya leo na uyafanyie
naamini utaona mabadiliko makubwa kwenye maisha yako.
Makala hii imeandikwa
na Suleiman khamis (Jaula).
Kwa mawasiliano zaidi : +255772800080, +255656400761.
E-mail: sulejaula@gmail.com, jaulasuleiman@gmail.com
Tovuti yetu: www.jaulanetwork.blogspot.com
EmoticonEmoticon